Peter Kenneth ajitosa tena kuwania ugavana Nairobi, akiwa huru

Mwanasiasa Peter Kenneth hii leo ametangaza rasmi azma yake ya kuwania kiti cha ugavana wa Nairobi kama mwaniaji huru. Kenneth ameelezea kutoridhishwa kwake na jinsi mchujo wa chama cha Jubilee uliendeshwa na kudai kuwa wizi wa kura za mchujo huo ulimnyima nafasi ya kuongoza mji wa Nairobi kwa kitiki ya chama hicho.

Mkakati huu mpya umeafikiwa baada ya mashauriano ya kina na wenyeji wa Nairobi, kenneth amesisitiza.
Kunadhifisha mji wa Nairobi, kuboresha huduma za kimsingi na uwajibikaji ni baadhi ya malengo ya mwaniaji huyo ambaye ameelezea imani yake kuwa wenyeji wa Nairobi watamchagua kuwa gavana katika kinyanganyiro cha uchaguzi mkuu

Tags:

Nairobi PETER KENNETH

Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories