Polycarp Igathe azinduliwa rasmi kama mgombea mwenza wa Sonko
Published on: May 17, 2017 10:19 (EAT)
Seneta wa Nairobi ambaye pia ni mwaniaji wa ugavana wa kaunti hii Mike Mbuvi Sonko hii leo alimzindua mgombea mwenza wake Polycarp Igathe katika makao makuu ya Jubilee.
Wawili hao walijipigia upato wakiahidi kurejesha vipande vya ardhi vilivyonyakuliwa sawiya na kupambana na ufisadi wanaosema umekithiri katika makau makuu ya kaunti ya nairobi.
Naibu Rais William Ruto aliashiria imani yake kuwa wawili hao wataendeleza jiji la Nairobi.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment