Rais Kenyatta akataa mwito wa mazungumzo na Raila

Rais Uhuru Kenyatta amepuuzilia mbali shinikizo la kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na kinara wa NASA Raila Odinga, kutafuta suluhu ya suitafahamu ya kisiasa inayolighubika taifa kwa sasa. Kenyatta anasema baada ya chaguzi mbili za urais na kuapishwa kwake kuhudumu kwa muhula wa pili, daftari la nipe nikupe za kisiasa limefungwa, na la sasa ni kufanikisha maendeleo ya kitaifa. Huku kauli yake ikipigwa jeki na naibu wake William Ruto, mabalozi wa kigeni, viongozi wa kidini na wale wa biashara wanasisitiza tiba ni mazungumzo tu.

Tags:

Uhuru kenyatta NASA dialogue raila Odinag

Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories