Rais Kenyatta azindua sehemu ya pili ya SGR
Published on: October 19, 2016 09:47 (EAT)
Rais Uhuru Kenyatta hii leo amekashifu wale wanaopinga mradi wa pili wa kujengwa kwa reli ya kisasa kuelekea Naivasha kutoka Nairobi na kusema kuwa swala la reli kupita katikati mwa Mbuga ya Nairobi itashughulikiwa ipasavyo. Rais Kenyatta aliyasema haya alipozindua mradi wa kujengwa kwa reli hiyo katika eneo la Em-bulbul, Ngong kaunti ya Kajiado. Mradi huo umekumbwa na utata huku kesi ikiwasilishwa mahakamani kupinga reli hiyo kupita ndani ya hifadhi ya wanyama ya Nairobi.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment