Rais Kenyatta azuru Marsabit, Samburu

Ziara ya Rais Kenyatta na naibu rais katika kaunti za Marsabit na Samburu zilishuhudia hali ya mshikemshike pale ambapo wafuasi wa wagombea ugavana walipopimana nguvu ya kisiasa  na kuwalazimu maafisa wa polisi kuingilia kati ili kuwatuliza. Wafuasi wa gavana Ukur Yattani na mgomea wa Jubilee Mohammud Mohammed walishikana mashati wote wakitafuta kutambuliwa kama mibabe wa kaunti ya Marsabit kwenye kampeni hiyo ya rais. Hata hivyo kampeni iliendelea walipotulizwa na rais kuzindua mradi wa barabara ya Moyale kuelekea Isiolo.

Tags:

Uhuru kenyatta JUBILEE Marsabit Ukur Yattani

Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories