Rais na naibu wake wakutana na wakuu wa bunge la kitaifa
Published on: December 04, 2017 08:19 (EAT)
Rais Uhuru Kenyatta amefanya mkutano na viongozi wakuu wa bunge la taifa katika ikulu ya Nairobi. Rais na naibu rais wamefanya mkutano na spika wa bunge la taifa Justin Muturi na kiongozi wa wengi bungeni Aden Duale kabla ya mkutano wa pamoja utakaowajumuisha spika wa seneti Ken Lusaka na kiongozi wa wengi kwenye seneti Kipchumba Murkomen. Mkutano huo unaarifiwa kujadili suala la kalenda ya bunge na uteuzi wa makamati.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment