Rufaa ya IEBC kuhusu kandarasi ya karatasi za kura kusikizwa Ijumaa
Published on: July 12, 2017 09:11 (EAT)
Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini, IEBC imewakilisha rasmi rufaa ya kupinga uamuzi wa mahakama kuu uliotolewa juma lililopita kusimamisha uchapishaji wa makaratasi ya kupigia kura na kampuni ya Al Ghurai kutoka dubai. IEBC inadai kuwa mahakama kuu haikuzingatia takwimu ikiwemo gharama itakayohitajika kuchapisha upya makaratasi hayo na kampuni nyingine. Hatma ya IEBC itajulikana Ijumaa wiki hii baada ya kuskizwa kwa kesi hiyo na majaji watano wa mahakama ya rufaa.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment