Ruto apuuzilia mbali wito wa Odinga wa ufadhili wa upinzani
Published on: October 22, 2016 10:07 (EAT)
Naibu Rais William Ruto ametupilia mbali ombi la kiongozi wa upinzani Raila Odinga kwa mataifa ya nje kutaka mataifa hayo kugharamia shughuli za vyama vya upinzani nchini. Odinga alitoa ombi hilo hapo jana akiwa Uingereza, lakini Ruto akizungumza katika shule ya upili ya Bukhalalire kaunti ya Busia amesema kuwa swala hilo ni njama ya kutafuta pesa kutoka nchi za nje ili kushawishi uchaguzi mkuu ujao.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment