Safaricom yaionya NASA dhidi ya kutoa vitisho

Afisa mkuu wa kampuni ya mawasiliano Bob Collymore amewataka wanasiasa kusita kuingiza masuala ya biashara na kampuni katika siasa akisema wataendelea kushirikiana na tume ya IEBC katika kandarasi ya uwasilishaji wa matokeo ya uchaguzi kwa njia ya kielektroniki. Collymore ambaye ameonekana kuulenga mrengo pinzani wa NASA ameapa kuwachukulia hatua wanasiasa husika endapo maafisa sita wa Safaricom waliotajwa na Raila Odinga watajipata taabani kutokana na ripoti kuwa walishiriki kuhujumu uchaguzi wa Agosti mwaka huu.

Tags:

Safaricom IEBC NASA Ezra Chiloba OT-MORPHO

Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories