Kiongozi wa chama cha NARC Charity Ngilu ameashiria kuwa huenda akajiunga na muungano wa CORD
Published on: October 14, 2016 11:34 (EAT)
Kiongozi wa chama cha NARC Charity Ngilu ameashiria kuwa huenda akajiunga na muungano wa CORD ili kuweza kumenyana na Jubilee katika kinyang’anyiro cha mwaka ujao. Katika mazishi ya mumewe kiongozi wa chama cha CCU Wavinya Ndeti, Ngilu aliashiria hayo na kusema kuwa uongozi wa juu wa CORD hauna wanawake na angehiari kurekebisha hayo. Haya yamejiri huku seneta wa Nairobi Mike Sonko akizomewa na kufurushwa na waombolezaji pale alipoanza kuwakosoa viongozi wa CORD.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment