Serikali yashinikizwa kutafuta njia mbadala ya reli
Published on: October 03, 2016 09:43 (EAT)
Serikali inazidi kushinikizwa itatafute njia mbadala ya kujenga njia ya reli ya kisasa ambayo inapitia katikati ya mbuga ya wanyama pori ya Nairobi. Kwa mara ya tatu sasa waakazi wa maeneo yanayopakana na mbuga hiyo wamefanya maandamano ya amani kupinga ujenzi huo kwa misingi kwamba utasababisha uharibifu wa mazingira na kuhatarisha maisha yao pamoja na kuwatatiza wanyama.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment