Uhuru azuru maeneo ya kaunti ya Nakuru
Published on: February 11, 2017 09:01 (EAT)
Rais Uhuru Kenyatta amewaeleza wapinzani wake ambao wamekuwa wakipinga ujenzi wa bwawa la Itare kuwa kelele zao hazitalemaza ujenzi huo. Akizunguka katika maeneo kadhaa ya kaunti ya Nakuru kuwarai wenyeji wajitokeze kusajiliwa kupiga kura, Rais Kenyatta amesema kuwa mradi huo unanuiwa kuhakikisha kuwa watu 800,000 wa kaunti hiyo wamepata maji ya kutosha. Naibu rais naye alikuwa katika kaunti ya Kajiado kuwatia shime wenyeji wajiandikishe kuwa wapigakura.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment