Uhuru: Ole wao watakaozua fujo Oktoba 26
Published on: October 20, 2017 08:54 (EAT)
Rais Uhuru Kenyatta amekariri kuwa marudio ya uchaguzi wa urais yatafanyika siku ya Alhamisi, kama ilivyoratibiwa na tume ya IEBC, licha ya kinara wa NASA Raila Odinga kujiondoa kwenye kinyang’anyiro. Huku wingu la suitafahamu likitanda, Kenyatta amewahakikishia maafisa wa IEBC na wananchi watakaoshiriki usalama wao, sawa na wafuasi wa nasa watakaohiari kushiriki maandamano kupinga zoezi hilo, kama walivyoagizwa na vigogo wao.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment