Upinzani wasema uko tayari kujadiliana na serikali kuhusu sheria ya uchaguzi
Published on: January 07, 2017 08:19 (EAT)
Viongozi wa upinzani sasa wanasema kuwa wako radhi kuzungumza kuhusu marekebisho kwenye sheria ya uchaguzi yanayoruhusu njia mbadala ya kuwatambua wapiga iwapo mitambo ya kieletroniki itafeli. Kinara mwenza wa CORD Moses Wetangula anasema kuwa wako radhi kufanya mazungumzo na kufanikisha kamati maalumu ya kutatua mzozo uliopo. Kiongozi wa Narc Kenya Martha Karua naye akipendekeza jopo na vyama mbalimbali almaarufu IPPG kuundwa kama ilivyofanyika hapo awali.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment