Utata wa kumteua mwaniaji urais wazuka
Je, muungano wa CORD uko sawa? Matamshi ya vinara wenza Kalonzo Musyoka na Moses Wetangula yalitoa taswira ya mkwaruzano unaochochewa na kitendawili cha atakayepeperusha bendera ya mungano huo katika kinyang’anyiro cha urais mwaka ujao. Huku ikidaiwa Musyoka na Wetangula huenda wakang’atuka na kumwacha Odinga solemba, wadadisi wanadokeza kuwa itambidi Odinga kuipanga upya safu yake, ili kuimarisha nafasi yake ya kumbwaga Rais Uhuru Kenyatta mwakani. Je, mustakabali wa cord ni upi?
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment