Vijana wa Akasha wakiri mashtaka ya ulanguzi wa mihadarati
Vijana wawili wa aliyekuwa mlanguzi wa dawa za kulevya Ibrahim Akasha wamekiri mashtaka ya kuhusika na ulanguzi wa mihadarati walipofikishwa mbele ya mahakama mjini New York.
Bakhtash na Ibrahim Akasha walifikishwa mbele ya mahakama ya Southern District mjini New York ambako msimamizi mkuu wa kukabiliana na mihadarati nchini Amisi Massa alikuwepo.
Kwa mujibu wa idara ya jinai, wawili hao walikiri mashtaka ya ulanguzi wa mihadarati, kuhusika na ufisadi na kuzuia kushafirishwa kwao kutoka humu nchini na pia njama ya kutumia bunduki kuendeleza biashara hiyo.
Wawili hao pamoja na raia wa Pakistan Gulam Hussein na raia mwingine wa India walihamishwa hadi nchini Marekani mwezi Januari mwaka 2017 baada ya kuzuiliwa mjini Mombasa.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment