Viongozi wa Jubilee waingia Narok
Published on: July 11, 2017 08:39 (EAT)
Rais Uhuru Kenyatta amesisitiza kuwa serikali haitawavumilia wanasiasa chochezi na kuwa ni sharti uchaguzi mkuu ufanyike tarehe 8 Agosti mwaka huu. Kadhalika muungano wa Jubilee hautawatuma wawakilishi kwenye vikao vya kutafuta kampuni itakayopewa zabuni ya kuchapisha karatasi za kupigia kura. Uhuru alizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Olmekenyu kaunti ya Narok alikoandamana na naibu wake pamoja na wanasiasa wengine wa Jubilee kuomba kura.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment