Viongozi wa kidini wakutana na madaktari
Mazungumzo yanaoongozwa na viongozi wa kidini kujaribu kutatua masuala tata yaliyosababisha mgomo wa madaktari yamekosa kuzaa matunda. Hii ni baada ya serikali, baraza la magavana na madaktari kukosa kuafikiana kuhusu suala la nyongeza ya mishahara na marupurupu. Waziri wa afya Dkt Cleopa Mailu ambaye alihudhuria mazungumzo hayo anasisitiza kuwa serikali haiwezi kugharamia zaidi ya asilimia 40 ya nyongeza huku baraza la magavana nalo likishikilia kuwa halitakubali mkataba wowote ikiwa madaktari hawajarejea kazini.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment