Wabunge kutoka pwani walalamikia kutengwa kwenye uongozi wa NASA
Published on: November 29, 2017 08:49 (EAT)
Muungano wa NASA hatimaye umewasilisha majina ya viongozi wao bungeni huku bunge likirejelea vikao vyake leo. Katika orodha hiyo, mbunge wa Suba Kusini John Mbadi akiteuliwa kuwa kiongozi wa wachache katika bunge la kitaifa na Seneta Moses Wetangula katika seneti. Hata hivyo kumezuka mgawanyiko huku wabunge kutoka pwani wakilalamikia kutengwa katika nyadhifa hizo.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment