Wabunge waendelea kupinga kupunguziwa mishahara
Published on: August 24, 2017 09:04 (EAT)
Rais Uhuru Kenyatta amewasuta wabunge wateule wanaoshinikiza mishahara yao kuongezwa kinyume na ratba iliyotolewa na tume ya kutathmini mishahara ya umma SRC. Rais aliyeonekana kughadhabishwa na viongozi hao ameapa kamwe hatatia saini kwa sheria yoyote inayonuia kuwaongeza wabunge mapato. Haya yanajiri huku baadhi ya wabunge wateule wakizidisha kilio chao wengine wakitisha mwenyekiti wa SRC Sarah Serem achukuliwe hatua wakidai amekiuka sheria.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment