Wabunge wateule wapinga pendekezo la kupunguziwa mishahara
Published on: August 23, 2017 09:03 (EAT)
Tume ya huduma za bunge PSC imesema haitatekeleza mapendekezo ya tume ya SRC ya kupunguza mishahara na marupurupu ya wabunge. Kwa mujibu wa mwakilishi wa wanawake wa kaunti ya Homa Bay Gladys Wanga, SRC haikutathmini kazi ya wabunge kabla ya kupunguza mishahara yao. Kwingineko IEBC hii leo imechapisha rasmi majina ya wabunge wote waliochaguliwa katika gazeti la serikali.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment