Wahasiriwa 54 wa fujo za kisiasa waliaga dunia – KNCHR yasema
Published on: November 03, 2017 08:34 (EAT)
Tume ya kitaifa kuhusu haki za kibinadamu KNCHR sasa inasema watu 54 walipoteza maisha yao kutokana na ghasia za kisiasa tangu uchaguzi wa Agosti hadi sasa. Mwenyekiti wa tume hiyo Kagwiria Mbogori anasema watu wao ni pamoja na 17 waliofariki mwezi uliopita kufuatia utumizi wa nguvu kupita kiasi na maafisa wa polisi walipokabiliana na wafuasi wa muungano wa NASA walipoandamana dhidi ya tume ya IEBC.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment