Wanasiasa waliohamia Jubilee watakiwa wajiuzulu
Published on: September 11, 2016 09:24 (EAT)
Wabunge na magavana wa CORD waliohamia chama kipya cha Jubilee wametakiwa kujiuzulu, na kutafuta mamlaka upya kupitia chama walichohamia. Kinara mwenza wa CORD Moses Wetang’ula amesema sheria ya vyama vya kisiasa ni bayana, kuwa huwezi kuwa mwanachama wa vyama viwili vya kisiasa kwa wakati mmoja. Msajili wa vyama Lucy Ndung’u anasisitiza hana mamlaka ya kuwaondoa kwenye sajili, wanachama wa vyama waliohamia Jubilee, bila ombi hilo kuwasilishwa kwake rasmi na vyama vilivyoathiriwa.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment