Washukiwa wa mihadarati wakamatwa punde baada ya kuachiliwa
Published on: March 02, 2017 09:28 (EAT)
Washukiwa wanne wa ulanguzi wa dawa za kulevya watasalia korokoroni hadi siku ya Jumatano juma lijalo, baada ya kukamatwa tena walipoachiliwa na mahakama kwa kigezo cha kuzuiliwa kinyume cha sheria. Nabil loo, bakari kali, lilian Martin na Stephen Mung’ira walishtakiwa kwa madai ya ulanguzi wa dawa za kulevya na ulanguzi wa fedha. Polisi wanadai waliwakamata wakiwa na kilo 15 za dawa aina ya heroine na kima cha shilingi milioni 18 pesa taslimu.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment