Watu 10 wafariki sehemu mbalimbali nchini
Published on: May 26, 2017 08:45 (EAT)
Watu 10 wamefariki katika ajali tatu tofauti za barabarani. Watu 5 wamefariki katika ajali katika barabara ya Kenol kuelekea Sagana na wengine wanne kutoka familia moja wakifariki katika ajali nyingine katika eneo la Nyando, kaunti ya Kisumu. Wakati huo huo mgombea wa kiti cha uwakilishi wadi katika wadi ya Itibo, eneo bunge la Mugirango Kaskazini, kaunti ya Nyamira Kefa Nyangatare amefariki papo hapo baada ya gari lake kukosa mwelekeo na kubingiria katika barabara ya Ikonge kuelekea magwagwa.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment