Wizara ya ardhi kuzindua mfumo wa malipo wa dijitali
Published on: December 03, 2017 08:32 (EAT)
Malipo yote ya ardhi, katika eneo la Nairobi na la kati mwa taifa hili yatafanyika kidijitali kuanzia kesho. Wakenya watahitajika kulipa kodi za ardhi kupitia mtandao wa ecitizen badala ya milolongo mirefu iliyoshuhudiwa katika makao makuu ya wizara ya ardhi hapo awali.
Kulingana na waziri wa ardhi Prof. Jacob Kaimenyi, hatua hii inanuiwa kuangamiza ufisadi uliozonga wizara ya ardhi kupitia watu wanaojidai mawakala wa wizara na kulaghai wananchi pesa.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment