Wizi wa mitihani : Shule ya St Theresa Girls Nakuru yafungwa

Shule ya upili ya kibinafsi ya st. Theresa senior, katika kaunti ya Nakuru imepokonywa cheti cha kuhudumu baada ya kupotikana na hatia ya  udanganyifu katika mtihani wa KCSE unaoendelea. Kupitia barua kwa usimamizi wa shule hiyo katibu katika wizara ya elimu Belio Kipsang’ ameamuru mwalimu mkuu kurejesha cheti cha usajili wa shule hiyo kwa mkurugenzi wa elimu wa kaunti ya Nakuru mara moja na kuifunga shule hiyo. Haya yanajiri huku waziri wa elimu Fred Matiangi akisema hakuna atakayesazwa iwapo atakiuka sheria.

Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories