Zoezi La Ajira Ya Polisi Kufanyika Jumatatu Ijayo
Published on: April 13, 2015 06:22 (EAT)
Idara ya kitaifa ya huduma ya polisi nchini imetangangaza upya hii leo shughuli ya mchujo wa makurutu wanaotarajia kujiunga na huduma hiyo itakayofanyika tarehe ishirini mwezi huu. Kulingana na tangazo hilo kwenye magazeti vijana wote wanaotarajia kujiunga wachukue fomu ya kujaza katika vituo vya polisi vilivyokaribu nao pamoja na afisi za machifu wao ama kituo cha huduma centre. Na kama mwanahabari wetu Alex Kubasu anavyotueleza, makurutu wote wameonywa dhidi ya udanganyifu au ufisadi wa aina yoyote.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment